Ayubu
20 Naye Sofari Mnaamathi akajibu, akasema:
2 “Ni kwa sababu hiyo fikira zangu zinazonifadhaisha zinanijibu,
Kwa sababu ya wasiwasi wangu wa ndani.
3 Nasikia himizo ambalo linanitusi;
Na roho ambayo haina uelewaji nilio nao mimi inanijibu.
5 Kwamba kilio cha shangwe cha watu waovu ni kifupi+
Na kushangilia kwa mwasi-imani ni kwa kitambo kidogo?
6 Ijapokuwa utukufu wake unapaa mbinguni+
Na kichwa chake chenyewe kinafika mawinguni,
7 Yeye anaangamia milele kama mavi yake;+
Wale wanaomwona watasema, ‘Yeye yuko wapi?’+
10 Wanawe watatafuta kibali cha watu wa hali ya chini,
Na mikono yake mwenyewe itarudisha vitu vyake vyenye thamani.+
11 Mifupa yake imekuwa yenye kujaa nguvu yake ya ujana,
Lakini italala pamoja naye katika mavumbi matupu.+
12 Ikiwa kilicho kibaya kina ladha tamu kinywani mwake,
Ikiwa anakiyeyusha chini ya ulimi wake,
13 Ikiwa anakihurumia wala hakiachi,
Na ikiwa anaendelea kukizuia katikati ya kaakaa lake,
14 Chakula chake hakika kitabadilishwa katika matumbo yake;
Kitakuwa nyongo ya swila ndani yake.
15 Amemeza mali, lakini ataitapika;
Mungu ataiondosha tumboni mwake.
18 Atairudisha mali yake aliyojipatia wala hataimeza;
Kama mali kutokana na biashara yake, lakini ambayo hataifurahia.+
19 Kwa maana ameponda vipande-vipande, amewaacha watu wa hali ya chini;
Ameinyakua nyumba ambayo hakuijenga.+
20 Kwa maana hakika hatajua starehe katika tumbo lake;
Hataponyoka kupitia vitu vyake vyenye kutamanika.+
21 Hakuna chochote kilichobaki kwa ajili yake ili kumeza;
Ndiyo sababu hali njema yake haitadumu.
23 Na iwe kwamba, ili kujaza tumbo lake,
Ataipeleka hasira yake inayowaka juu yake+
Naye atainyesha juu yake, ndani ya matumbo yake.
25 Mshale utachomoka kupitia mgongo wake,
Na silaha inayong’aa kupitia nyongo yake;+
Vitu vyenye kuogopesha vitaenda juu yake.+
26 Giza lote litawekwa akiba kwa ajili ya hazina zake;
Moto ambao hakuna mtu aliyeupepea utamteketeza;+
Mambo yatamwendea vibaya mwenye kuokoka aliye katika hema lake.