Ayubu
19 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Ninyi mtaendelea kunikasirisha nafsi yangu mpaka wakati gani+
Na kuendelea kuniponda kwa maneno?+
6 Jueni, basi, kwamba Mungu mwenyewe amenipotosha,
Naye ameuzungusha wavu wake wa kuwindia juu yangu.+
7 Tazama! Ninaendelea kupaaza sauti, ‘Jeuri!’ lakini sipati jibu lolote;+
Naendelea kulia nipewe msaada, lakini hakuna haki.+
8 Amezuia pito langu kwa ukuta wa mawe,+ nami siwezi kupita;
Naye anaweka giza katika barabara zangu.+
10 Ananibomoa pande zote, nami naenda zangu;
Naye anang’oa tumaini langu kama mti.
12 Vikosi vyake vinakuja kwa muungano na kujenga njia yao juu yangu,+
Nao wanapiga kambi kuzunguka hema langu.
14 Watu ninaofahamiana nao wamekoma kuwapo,+
Na wale ninaowajua wamenisahau,
15 Wale wanaokaa wakiwa wageni nyumbani mwangu;+ na vijakazi wangu wananiona kuwa mgeni;
Nimekuwa mgeni kwelikweli machoni pao.
16 Nimemwita mtumishi wangu, lakini hajibu.
Ninaendelea kumwomba huruma kwa kinywa changu mwenyewe.
21 Mnionyeshe kibali kidogo, mnionyeshe kibali kidogo, enyi rafiki zangu,+
Kwa kuwa mkono wenyewe wa Mungu umenigusa.+
23 Laiti sasa maneno yangu yangekuwa yameandikwa!
Laiti yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
25 Nami mwenyewe najua vema kwamba mkombozi wangu+ yuko hai,
Na kwamba, akija baada yangu, yeye atasimama+ juu ya mavumbi.
26 Na baada ya ngozi yangu, ambayo wameichuna,—hii!
Lakini ijapokuwa kupungua kwa mwili wangu nitamwona Mungu,
27 Ambaye mimi mwenyewe nitamwona,+
Na ambaye macho yangu hakika yatamwona, bali si mgeni.
Figo zangu zimeisha nguvu ndani yangu kabisa.