Zaburi
Zaburi
KITABU CHA KWANZA
1 Mwenye furaha+ ni mtu ambaye hakutembea katika shauri la waovu,+
Na katika njia ya watenda-dhambi hakusimama,+
Na katika kiti cha wenye dhihaka hakuketi.+
2 Bali mapendezi yake ni katika sheria ya Yehova,+
Naye huisoma sheria yake kwa sauti ya chini mchana na usiku.+
3 Naye hakika atakuwa kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji,+
Ambao hutoa matunda yake katika majira yake+
Na ambao majani yake hayanyauki,+
Na kila jambo analofanya litafanikiwa.+