2 Kwa nini mataifa yamekuwa na fujo+
Na vikundi vya mataifa vimeendelea kusema jambo la upuuzi?+
2 Wafalme wa dunia wanachukua msimamo wao+
Nao maofisa wakuu wamejikusanya pamoja kama mtu mmoja+
Dhidi ya Yehova+ na dhidi ya mtiwa-mafuta wake,+
3 Wakisema: “Na tuzikate pingu zao+
Na kuzitupa kamba zao mbali nasi!”+
4 Yule anayeketi mbinguni+ atacheka;
Yehova mwenyewe atawadharau.+
5 Wakati huo atasema nao katika hasira yake+
Na katika ghadhabu yake atawafadhaisha,+
6 Na kusema: “Mimi, naam, mimi nimemweka mfalme wangu+
Juu ya Sayuni,+ mlima wangu mtakatifu.”+
7 Acheni nirejezee agizo la Yehova;
Yeye ameniambia: “Wewe ni mwanangu;+
Mimi, leo, nimekuwa baba yako.+
8 Niombe,+ ili nikupe mataifa yawe urithi wako+
Na miisho ya dunia iwe miliki yako mwenyewe.+
9 Utawavunja kwa fimbo ya chuma ya enzi,+
Utawavunja vipande-vipande, kama chombo cha mfinyanzi.”+
10 Na sasa, enyi wafalme, onyesheni ufahamu;
Kubalini kurekebishwa, enyi waamuzi wa dunia.+
11 Mtumikieni Yehova kwa woga+
Na mshangilie kwa kutetemeka.+
12 Mbusuni mwana,+ ili Yeye asikasirike
Nanyi msiangamizwe kutoka njiani,+
Kwa maana hasira yake huwaka kwa urahisi.+
Wenye furaha ni wale wote wanaomkimbilia.+