Ya Daudi. Muziki.
24 Dunia na vyote vinavyoijaza ni vya Yehova,+
Nchi yenye kuzaa na wale wanaokaa ndani yake.+
2 Kwa maana yeye ameiweka imara juu ya bahari,+
Naye huiweka imara juu ya mito.+
3 Ni nani anayeweza kuupanda mlima wa Yehova,+
Na ni nani anayeweza kusimama katika mahali pake patakatifu?+
4 Yeyote asiye na hatia katika mikono yake na aliye safi moyoni,+
Ambaye hajaitendea nafsi Yangu kwa ubatili mtupu,+
Wala kuapa kwa udanganyifu.+
5 Atachukua baraka kutoka kwa Yehova+
Na uadilifu kutoka kwa Mungu wake wa wokovu.+
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wanaomtafuta,
Cha wale wanaoutafuta uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.+ Sela.
7 “Inueni vichwa vyenu, enyi malango,+
Na mjiinue, enyi miingilio ya kudumu,+
Ili Mfalme mtukufu apate kuingia!”+
8 “Basi, Mfalme huyo mtukufu ni nani?”+
“Yehova mwenye nguvu na mwenye uwezo,+
Yehova mwenye uwezo katika vita.”+
9 “Inueni vichwa vyenu, enyi malango;+
Naam, viinueni juu, enyi miingilio ya kudumu,
Ili Mfalme mtukufu apate kuingia!”+
10 “Basi, yeye ni nani, huyo Mfalme mtukufu?”
“Yehova wa majeshi—yeye ndiye Mfalme mtukufu.”+ Sela.