Muziki wa Daudi.
29 Mhesabieni Yehova, enyi wana wa wenye nguvu,
Mhesabieni Yehova utukufu na nguvu.+
2 Mhesabieni Yehova utukufu wa jina lake.+
Mwinamieni Yehova katika pambo takatifu.+
3 Sauti ya Yehova iko juu ya maji;+
Mungu mtukufu+ mwenyewe amenguruma.+
Yehova yuko juu ya maji mengi.+
4 Sauti ya Yehova ina nguvu;+
Sauti ya Yehova ni yenye fahari.+
5 Sauti ya Yehova inaivunja mierezi;
Naam, Yehova anaivunja vipande-vipande mierezi ya Lebanoni,+
6 Naye huifanya irukeruke kama ndama,+
Lebanoni na Sirioni+ kama wana wa ng’ombe-mwitu.
7 Sauti ya Yehova inapasua kwa miali ya moto;+
8 Sauti ya Yehova huifanya nyika itetemeke,+
Yehova huifanya nyika ya Kadeshi+ itetemeke.
9 Sauti ya Yehova huwafanya paa watetemeke kwa maumivu ya kuzaa+
Na kuivua kabisa misitu.+
Na katika hekalu lake kila mmoja anasema: “Utukufu!”+
10 Yehova ameketi juu ya gharika;+
Na Yehova huketi akiwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo.+
11 Yehova atawapa watu wake nguvu kwelikweli.+
Yehova atawabariki kwa amani watu wake.+