Zaburi
Muziki. Wimbo wa kuzindua nyumba.+ Wa Daudi.
30 Nitakutukuza wewe, Ee Yehova, kwa maana umeniinua+
Nawe hukuwaruhusu adui zangu washangilie juu yangu.+
2 Ee Yehova Mungu wangu, nilikulilia unisaidie, nawe ukaniponya.+
3 Ee Yehova, umeitoa nafsi yangu kutoka katika Kaburi;*+
Umeendelea kuniweka nikiwa hai, ili nisipate kushuka ndani ya shimo.+
5 Kwa sababu kuwa chini ya hasira yake ni kwa muda kidogo tu,+
Kuwa chini ya nia yake njema ni kwa muda wote wa maisha.+
Huenda kilio kikakaa wakati wa jioni,+ lakini asubuhi kuna vigelegele vya shangwe.+
7 Ee Yehova, umeusimamisha mlima wangu katika nguvu kwa nia yako njema.+
Uliuficha uso wako; nikawa na wasiwasi.+
9 Damu yangu ina faida gani ninaposhuka katika shimo?+
Je, mavumbi yatakusifu wewe?+ Je, yatasema juu ya ukweli wako?+