26 Naye akasema: “Ikiwa utaisikiliza kwa makini sauti ya Yehova Mungu wako na kufanya lililo sawa machoni pake na kutega sikio usikie amri zake na kushika masharti yake yote,+ sitaweka juu yako yoyote ya magonjwa yale niliyoweka juu ya Wamisri;+ kwa sababu mimi ni Yehova anayekuponya.”+
5 “Rudi, umwambie Hezekia kiongozi+ wa watu wangu, ‘Yehova, Mungu+ wa Daudi babu yako, amesema hivi: “Nimeisikia+ sala+ yako. Nimeyaona machozi+ yako. Tazama, ninakuponya.+ Siku ya tatu utapanda kwenda katika nyumba ya Yehova.+