Kwa kiongozi wa vinanda katika sauti ya nane ya chini.+ Muziki wa Daudi.
6 Ee Yehova, katika hasira yako usinikaripie,+
Na katika ghadhabu yako usinirekebishe.+
2 Nionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana mimi ninafifia.+
Niponye,+ Ee Yehova, kwa maana mifupa yangu imesumbuka.
3 Naam, nafsi yangu imesumbuka sana;+
Nawe, Ee Yehova—hata wakati gani?+
4 Urudi,+ Ee Yehova, uokoe nafsi yangu;+
Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako zenye upendo.+
5 Kwa maana katika kifo wewe hutajwi;+
Katika Kaburi ni nani atakayekusifu?+
6 Nimechoshwa na kuugua kwangu;+
Usiku kucha nafanya kitanda changu kilowane;+
Kwa machozi yangu nafanya kitanda changu kifurike.+
7 Kutokana na masumbufu jicho langu limekuwa dhaifu,+
Limezeeka kwa sababu ya wale wote wanaonionyesha uadui.+
8 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mnaozoea kutenda mambo yenye kuumiza,+
Kwa maana hakika Yehova atasikia sauti ya kulia kwangu.+
9 Yehova mwenyewe atasikia kwelikweli ombi langu la kutaka kibali;+
Yehova ataikubali sala yangu.+
10 Adui zangu wote wataona aibu+ sana na kuwa na wasiwasi;
Watageuka, wataona aibu ghafula.+