Zaburi
Wimbo wa huzuni wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kuhusu maneno ya Kushi Mbenyamini.
7 Ee Yehova Mungu wangu,+ nimekukimbilia wewe.+
Uniokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unikomboe,+
2 Ili mtu yeyote asiirarue nafsi yangu vipande-vipande kama simba anavyofanya,+
Kuninyakua wakati ambapo hakuna mkombozi.+
3 Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimefanya hili,+
Ikiwa kuna ukosefu wowote wa haki katika mikono yangu,+
4 Ikiwa nimemlipa ubaya yule anayenipa thawabu,+
Au ikiwa nimempora yeyote anayenionyesha uadui bila kufanikiwa,+
5 Adui na aifuatilie nafsi yangu+
Naye afikie na kukanyagia chini uhai wangu
Na kufanya utukufu wangu ukae mavumbini. Sela.
6 Usimame, Ee Yehova, katika hasira yako;+
Uinuke katika milipuko ya ghadhabu ya wale wanaonionyesha uadui,+
Na uamke kwa ajili yangu,+ kwa maana umetoa amri kwa ajili ya hukumu.+
7 Nalo kusanyiko la vikundi vya mataifa na likuzunguke,
Nawe urudi juu dhidi yake.
8 Yehova mwenyewe atavihukumu vikundi vya watu.+
Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wangu+
Na kulingana na utimilifu+ wangu ulio ndani yangu.
10 Ngao yangu iko juu ya Mungu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+
12 Ikiwa mtu yeyote hatarudi,+ Yeye ataunoa upanga wake,+
Hakika ataupinda upinde wake, naye atauweka tayari ili kufyatuliwa.+
14 Tazama! Kuna mtu aliye na mimba ya jambo lenye kuumiza,+
Naye amechukua mimba ya taabu na hatakosa kuzaa uwongo.+