Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
6 Nawachukia wale wanaoonyesha kujali sanamu zisizo na faida, za ubatili;+
Lakini mimi, namtegemea Yehova.+
7 Nitakuwa na shangwe na kushangilia katika fadhili zako zenye upendo,+
Kwa kuwa umeona mateso yangu;+
Umejua juu ya taabu za nafsi yangu.+
9 Unionyeshe kibali, Ee Yehova, kwa maana niko katika dhiki kali.+
Mambo yenye kukera yamefanya jicho langu liwe dhaifu,+ naam, nafsi yangu na tumbo langu.+
10 Kwa maana uhai wangu umefikia mwisho kwa huzuni,+
Na miaka yangu kwa kuugua.+
Kwa sababu ya kosa langu nguvu zangu zimejikwaa,+
Na mifupa yangu imekuwa dhaifu.+
11 Nimekuwa shutuma+ kwa wale wote wanaonionyesha uadui,+
Na nimekuwa hivyo hata zaidi kwa jirani zangu,+
Na kitu chenye kutia hofu kwa rafiki zangu.+
Wakati wanaponiona nje, wamenikimbia.+
12 Nimesahaulika kama mtu ambaye amekufa na ambaye hayumo moyoni;+
Nimekuwa kama chombo kilichoharibika;+
13 Kwa maana nimeisikia habari mbaya kutoka kwa wengi,+
Pande zote kukiwa na woga.+
Wanapoungana kama kitu kimoja dhidi yangu,+
Wanapanga hila ili kuiondoa nafsi yangu.+
15 Nyakati zangu ziko katika mkono wako.+
Unikomboe kutoka katika mkono wa adui zangu na kutoka kwa wale wanaonifuatilia.+
18 Midomo inayosema uwongo na ishindwe kusema,+
Inayosema mambo dhidi ya mwadilifu,+ bila kujizuia katika majivuno na dharau.+
19 Jinsi ulivyo mwingi wema wako,+ ambao umewawekea hazina wale wanaokuogopa!+
Ambao umewapa wale wanaokukimbilia wewe,
Mbele ya wana wa binadamu.+
20 Utawaficha katika mahali pa siri pa uso wako+
Mbali na ukusanyikaji pamoja wa watu.+
Utawaficha katika kibanda chako mbali na kugombana kwa ndimi.+
22 Mimi nilisema hivi niliposhikwa na wasiwasi:+
“Hakika nitaangamizwa kutoka mbele za macho yako.”+
Bila shaka umeisikia sauti ya kusihi kwangu nilipokulilia unisaidie.+