30 Na mimea yote ya majani nimetoa iwe chakula+ kwa kila mnyama-mwitu wa dunia na kila kiumbe kinachoruka cha mbinguni na kila kitu kinachotembea juu ya dunia ambacho ndani yake mna uhai ukiwa nafsi.” Ikawa hivyo.
11 Kwa maana nafsi ya mwili iko katika damu,+ nami mwenyewe nimeiweka juu ya madhabahu ili ninyi mfanye upatanisho+ kwa ajili ya nafsi zenu, kwa sababu damu+ ndiyo hufanya upatanisho+ kupitia nafsi iliyo ndani yake.
14 Kwa maana nafsi ya kila namna ya mwili ni damu yake kwa nafsi iliyo ndani yake. Basi niliwaambia wana wa Israeli: “Hamtakula damu ya mwili wa namna yoyote, kwa sababu nafsi ya kila mwili wa namna yoyote iko katika damu yake.+ Mtu yeyote atakayeila atakatiliwa mbali.”+