21 Naye Yehova alikuwa akienda mbele yao wakati wa mchana katika nguzo ya wingu ili kuwaongoza njiani,+ na wakati wa usiku katika nguzo ya moto ili kuwapa nuru ya kwenda wakati wa mchana na wakati wa usiku.+
5 Hakuna yeyote atakayesimama imara mbele yako siku zote za maisha yako.+ Nitakuwa pamoja nawe,+ kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa. Sitakutupa wala kukuacha kabisa.+
9 Wakati wa taabu zao zote hilo lilimtaabisha.+ Na mjumbe wake binafsi akawaokoa.+ Katika upendo wake na katika huruma yake yeye mwenyewe aliwakomboa,+ naye akawainua na kuwachukua siku zote za zamani za kale.+