2 Na Yehova akamwambia Musa: “Sema na Haruni ndugu yako, asiwe akija nyakati zote katika mahali patakatifu+ ndani ya pazia,+ mbele ya kifuniko kilicho juu ya Sanduku, asije akafa;+ kwa sababu nitaonekana katika wingu+ juu ya kifuniko+ hicho.
14 “Naye atachukua sehemu ya damu ya ng’ombe-dume+ na kuitapanya kwa kidole chake mbele ya kifuniko upande wa mashariki, naye atatapanya+ sehemu ya damu hiyo kwa kidole chake mara saba mbele ya kifuniko.+
11 Na Daudi akampa Sulemani mwana wake ramani ya ujenzi+ wa ukumbi+ na ya nyumba zake na ya maghala+ yake na madari+ yake na ya vyumba vyake vya ndani vyenye giza na nyumba ya kifuniko cha upatanisho;+