12 “Nimeyasikia manung’uniko ya wana wa Israeli.+ Sema nao, na kuwaambia, ‘Katikati ya zile jioni mbili mtakula nyama na asubuhi mtashiba mkate;+ nanyi hakika mtajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’”+
3 Katika siku ya kumi na nne ya mwezi huu katikati ya zile jioni mbili+ mtaitayarisha katika wakati wake uliowekwa. Kulingana na sheria zake zote na utaratibu wake wote wa kawaida mtaitayarisha.”+
6 Bali mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua ili jina lake likae,+ hapo utatoa dhabihu ya pasaka wakati wa jioni mara tu baada ya jua kutua,+ wakati uliowekwa wa kutoka kwenu Misri.