2 Naye atauweka mkono wake juu ya kichwa+ cha toleo lake, nalo litachinjwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano; nao wana wa Haruni, makuhani, watainyunyiza damu yake kwenye madhabahu kuizunguka pande zote.
4 Naye atamleta ng’ombe huyo kwenye mwingilio wa hema la mkutano+ mbele za Yehova na kuuweka mkono wake juu ya kichwa cha ng’ombe huyo,+ naye atamchinja ng’ombe huyo mbele za Yehova.
21 Na Haruni ataweka mikono yake miwili+ juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai na kuungama+ juu yake makosa+ yote ya wana wa Israeli na maasi yao yote na dhambi+ zao zote, naye atayaweka juu ya kichwa cha yule mbuzi+ na kumpeleka mpaka nyikani+ kwa mkono wa mtu aliye tayari.+
6 Sisi sote tumeenda huku na huku kama kondoo;+ sisi tumegeuka kwenda kila mmoja kwenye njia yake; na Yehova amefanya kosa letu sote likutane na huyo.+
24 Yeye mwenyewe alichukua dhambi+ zetu katika mwili wake mwenyewe juu ya mti,+ ili tuachane kabisa na dhambi+ na kuishi kwa uadilifu. Na “kwa mapigo yake mliponywa.”+