Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 53:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu katikati ya wengi,+ naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,+ kwa sababu aliimwaga nafsi yake mpaka kufa,+ naye alihesabiwa pamoja na wakosaji;+ naye mwenyewe aliichukua dhambi ya watu wengi,+ aliingilia kati kwa ajili ya wakosaji.+

  • Yohana 1:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Siku iliyofuata alimwona Yesu akimjia, naye akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi+ ya ulimwengu!+

  • Waroma 15:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe;+ bali kama ilivyoandikwa: “Shutuma za wale waliokuwa wanakushutumu zimeniangukia.”+

  • Waefeso 1:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa njia yake tuna kuachiliwa huru kwa njia ya fidia kupitia damu+ ya huyo, ndiyo, msamaha+ wa makosa yetu, kulingana na utajiri wa fadhili zake zisizostahiliwa.+

  • Waebrania 9:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 vivyo hivyo pia Kristo alitolewa+ mara moja kwa wakati wote ili kubeba dhambi za wengi;+ na mara ya pili+ atakapotokea+ itakuwa ni bila dhambi+ na kwa wale wanaomtazamia kwa bidii kwa ajili ya wokovu wao.+

  • 1 Petro 2:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Yeye mwenyewe alichukua dhambi+ zetu katika mwili wake mwenyewe juu ya mti,+ ili tuachane kabisa na dhambi+ na kuishi kwa uadilifu. Na “kwa mapigo yake mliponywa.”+

  • 1 Yohana 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Mnajua pia kwamba huyo alifunuliwa ili kuondolea mbali dhambi zetu,+ na hakuna dhambi+ ndani yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki