8 Nami nitawatakasa kutoka katika kosa lao lote ambalo kupitia hilo wamenitendea dhambi,+ nami nitayasamehe makosa yao yote ambayo kupitia hayo wamenitendea dhambi na ambayo kupitia hayo wamenikosea.+
25 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi;+ nami nitawasafisha ninyi kutokana na uchafu+ wenu wote na kutokana na sanamu zenu zote za mavi.+
14 je, si zaidi damu+ ya Kristo, ambaye kupitia roho inayodumu milele alijitoa+ mwenyewe bila dosari kwa Mungu, itazisafisha+ dhamiri zetu kutoka katika matendo yaliyokufa+ ili tutoe utumishi mtakatifu+ kwa Mungu aliye hai?
2 Kama sivyo, je, dhabihu hazingekoma kutolewa, kwa sababu wale wanaotoa utumishi mtakatifu ambao walikuwa wamesafishwa mara moja kwa wakati wote hawangekuwa na ufahamu wa dhambi tena?+