Waefeso
5 Kwa hiyo, iweni waigaji wa Mungu,+ kama watoto wapendwa, 2 na endeleeni kutembea katika upendo,+ kama vile Kristo pia alivyowapenda ninyi+ na kujitoa mwenyewe kwa ajili yenu kuwa toleo+ na dhabihu kwa Mungu ili kuwa harufu tamu.+
3 Uasherati+ na ukosefu wa usafi wa kila namna au pupa+ visitajwe hata kidogo katikati yenu,+ kama inavyowafaa watu watakatifu;+ 4 wala mwenendo wa aibu+ wala maneno ya kipumbavu wala mizaha michafu,+ mambo yasiyofaa, lakini badala ya hayo, utoaji wa shukrani.+ 5 Kwa maana mnajua hili, nanyi mnalitambua wenyewe, kwamba hakuna mwasherati+ au mtu asiye safi au mtu mwenye pupa+—maana yake ni kuwa mwabudu-sanamu—aliye na urithi wowote katika ufalme wa Kristo na wa Mungu.+
6 Mtu yeyote asiwadanganye ninyi kwa maneno matupu,+ kwa maana kwa sababu ya mambo yaliyotangulia kusemwa ghadhabu ya Mungu inakuja juu ya wana wa kutotii.+ 7 Kwa hiyo msishirikiane pamoja nao;+ 8 kwa maana wakati mmoja ninyi mlikuwa giza,+ bali sasa ninyi ni nuru+ kuhusiana na Bwana. Endeleeni kutembea kama watoto wa nuru, 9 kwa maana matunda ya nuru yana kila namna ya wema na uadilifu na kweli.+ 10 Endeleeni kuhakikisha lile linalokubalika+ kwa Bwana; 11 na mwache kushirikiana+ pamoja nao katika matendo yasiyozaa matunda, ambayo ni ya giza,+ lakini badala yake muwe hata mkiyakaripia,+ 12 kwa maana mambo ambayo wao hutenda katika siri hata kuyasimulia ni aibu.+ 13 Basi mambo yote yanayokaripiwa+ yanafunuliwa na nuru, kwa maana kila jambo linalofunuliwa+ ni nuru. 14 Kwa hiyo yeye anasema: “Amka,+ Ee mwenye kulala usingizi, na ufufuke kutoka kwa wafu,+ na Kristo atakuangaza.”+
15 Kwa hiyo endeleeni kuangalia sana kwamba jinsi mnavyotembea+ si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima, 16 mkijinunulia wakati unaofaa,+ kwa sababu siku hizi ni zenye uovu.+ 17 Kwa hiyo mwache kuwa wenye kukosa akili, bali endeleeni kufahamu+ yale yaliyo mapenzi+ ya Yehova. 18 Pia, msiwe mkilewa+ divai, ambayo ina upotovu ndani yake,+ bali endeleeni kujazwa na roho,+ 19 mkijisemesha kwa zaburi+ na sifa+ kwa Mungu na nyimbo za kiroho, mkiimba+ na kupiga muziki+ katika mioyo yenu kwa Yehova, 20 katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo mkimtolea shukrani+ sikuzote Mungu na Baba yetu kwa ajili ya mambo yote.
21 Jitiisheni kwa mmoja na mwenzake+ katika kumwogopa Kristo. 22 Wake na wajitiishe+ kwa waume zao kama kwa Bwana, 23 kwa sababu mume ni kichwa cha mke+ wake kama vile Kristo pia alivyo kichwa cha kutaniko,+ yeye akiwa mwokozi wa mwili huu. 24 Kwa kweli, kama kutaniko linavyojitiisha kwa Kristo, vivyo hivyo wanawake pia na wajitiishe kwa waume zao katika mambo yote.+ 25 Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu,+ kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake,+ 26 ili alitakase,+ akilisafisha na kuliosha kwa maji kwa njia ya neno,+ 27 ili kujipa mwenyewe kutaniko likiwa na fahari,+ likiwa bila doa au kunyanzi au lolote la mambo hayo, bali ili liwe takatifu na bila dosari.+
28 Vivyo hivyo waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Yeye anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, 29 kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza+ kwa upendo, kama vile Kristo pia anavyolitendea kutaniko, 30 kwa sababu sisi ni viungo vya mwili wake.+ 31 “Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”+ 32 Siri hii takatifu+ ni kubwa. Sasa ninasema kwa habari ya Kristo na kutaniko.+ 33 Hata hivyo, pia, kila mtu mmoja-mmoja kati yenu na ampende hivyo mke wake+ kama vile anavyojipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, mke anapaswa kumheshimu+ sana mume wake.