21Na Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Ongea na makuhani, wana wa Haruni, nawe uwaambie, ‘Kwa ajili ya nafsi iliyokufa, mtu yeyote asijitie unajisi katikati ya watu wake.+
2 “Amuru wana wa Israeli kwamba wamtoe nje ya kambi kila mtu mwenye ukoma+ na kila mtu mwenye mtiririko unaotoka+ na kila mtu asiye safi kutokana na nafsi iliyokufa.+
9 Lakini ikiwa yeyote anayekufa atakufa ghafula kando yake+ hivi kwamba awe amekitia unajisi kichwa cha Unadhiri wake, basi lazima anyoe+ kichwa chake katika siku ya kuthibitisha utakaso wake. Katika siku ya saba anapaswa kukinyoa.
6 Sasa kukawa na watu ambao walikuwa wamekuwa najisi kwa sababu ya nafsi+ ya binadamu hivi kwamba hawakuweza kuitayarisha dhabihu ya pasaka katika siku hiyo. Kwa hiyo wakaenda mbele ya Musa na Haruni katika siku hiyo.+