28“Na wewe, mlete karibu nawe Haruni ndugu yako na wanawe pamoja naye kutoka katikati ya wana wa Israeli ili awe kuhani kwangu,+ Haruni,+ Nadabu na Abihu,+ Eleazari na Ithamari,+ wana wa Haruni.
5 Na itatukia kwamba mtu nitakayemchagua,+ fimbo yake itachipuka, nami nitakomesha manung’uniko+ ya wana wa Israeli juu yangu, ambayo wananung’unika juu yenu.”+
28 Naye alichaguliwa kwa ajili yangu kutoka kwa makabila yote ya Israeli,+ awe kuhani na kupanda juu ya madhabahu+ yangu ili afukize moshi wa dhabihu, avae efodi mbele zangu, ili niipe nyumba ya babu yako matoleo yote ya wana wa Israeli yaliyotolewa kwa njia ya moto.+