105 Mshukuruni Yehova, liitieni jina lake,+
Yajulisheni matendo yake katikati ya vikundi vya watu.+
2 Mwimbieni, mpigieni muziki,+
Jishughulisheni na kazi zake zote za ajabu.+
3 Jisifuni katika jina lake takatifu.+
Moyo wa wale wanaomtafuta Yehova na ushangilie.+
4 Mtafuteni Yehova na nguvu zake.+
Utafuteni uso wake daima.+
5 Kumbukeni kazi zake za ajabu ambazo amefanya,+
Miujiza yake na maamuzi ya hukumu ya kinywa chake,+
6 Enyi uzao wa Abrahamu mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Maamuzi yake ya hukumu yako duniani pote.+
8 Amelikumbuka agano lake mpaka wakati usio na kipimo,+
Neno ambalo aliamuru, mpaka vizazi elfu,+
9 Agano ambalo alifanya na Abrahamu,+
Na ahadi yake yenye kiapo aliyomwapia Isaka,+
10 Kiapo ambacho alikiendeleza kikiwa sharti kwa Yakobo,
Kama agano lenye kudumu kwa Israeli mpaka wakati usio na kipimo,+
11 Akisema: “Nitakupa wewe nchi ya Kanaani+
Kuwa fungu la urithi wenu.”+
12 Huo ni wakati walipokuwa wachache,+
Naam, wachache sana, na wakaaji wageni humo.+
13 Nao wakaendelea kutembea kutoka kwa taifa moja mpaka kwa taifa lingine,+
Kutoka katika ufalme mmoja mpaka kwa kikundi kingine cha watu.+
14 Hakumruhusu binadamu yeyote awapunje,+
Bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao,+
15 Akisema: “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,+
Wala msiwatendee manabii wangu lolote lililo baya.”+
16 Naye akaitisha njaa juu ya nchi;+
Alivunja kila fimbo ambayo mikate ya mviringo ilining’inizwa juu yake.+
17 Akamtuma mtu mbele yao,
Ambaye aliuzwa awe mtumwa, Yosefu.+
18 Wakaitesa miguu yake kwa pingu,+
Nafsi yake ikaingia katika vyuma;+
19 Mpaka wakati neno lake lilipotimia,+
Maneno ya Yehova mwenyewe yakamsafisha.+
20 Mfalme akatuma watu ili apate kumwachilia,+
Mtawala wa vikundi vya watu, ili apate kumfungua.
21 Akamweka kuwa bwana wa nyumba yake+
Na kuwa mtawala juu ya mali yake yote,+
22 Ili awafunge wakuu wake kama inavyopenda nafsi yake+
Na ili apate kuwafundisha hekima hata wanaume wake wazee.+
23 Na Israeli akaingia Misri,+
Na Yakobo mwenyewe akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.+
24 Naye akaendelea kuwafanya watu wake wazaane sana,+
Na hatua kwa hatua akawafanya kuwa wenye uwezo kuliko adui zao.+
25 Akaiacha mioyo yao ibadilike ili kuwachukia watu wake,+
Ili wajiendeshe kwa ujanja juu ya watumishi wake.+
26 Alimtuma Musa mtumishi wake,+
Haruni aliyekuwa amemchagua.+
27 Wakaweka kati yao mambo ya ishara zake,+
Na miujiza katika nchi ya Hamu.+
28 Alituma giza na kwa hiyo akafanya kuwe na giza;+
Nao hawakuyaasi maneno yake.+
29 Aliyabadili maji yao yakawa damu,+
Akawaua samaki wao.+
30 Nchi yao ikajaa vyura,+
Katika vyumba vya ndani vya wafalme.
31 Alisema mainzi waingie,+
Na chawa katika maeneo yao yote.+
32 Aliifanya mvua yao iwe mvua ya mawe,+
Moto wenye mwali juu ya nchi.+
33 Naye akapiga mizabibu yao na mitini yao
Na kuvunja miti ya eneo lao.+
34 Akasema nzige waingie,+
Na nzige wachanga, wasio na hesabu.+
35 Nao wakala mimea yote katika nchi yao;+
Pia wakala mazao ya udongo wao.
36 Naye akapiga na kuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+
Mwanzo wa nguvu zao zote za uzazi.+
37 Naye akaanza kuwatoa nje wakiwa na fedha na dhahabu;+
Na katikati ya makabila yake hapakuwa na yeyote mwenye kujikwaa.
38 Misri ilishangilia walipoondoka,
Kwa maana hofu yao ilikuwa imewaangukia.+
39 Alitandaza wingu lifunike,+
Na moto utoe nuru wakati wa usiku.+
40 Waliomba, naye akaleta kware,+
Na kwa mkate kutoka mbinguni akaendelea kuwashibisha.+
41 Alifungua mwamba, na maji yakaanza kutiririka;+
Nayo yakapita katika maeneo yasiyo na maji kama mto.+
42 Kwa maana alilikumbuka neno lake takatifu kwa Abrahamu mtumishi wake.+
43 Kwa hiyo akawatoa watu wake kwa kushangilia,+
Wachaguliwa wake kwa vigelegele vya shangwe.+
44 Na hatua kwa hatua akawapa nchi za mataifa,+
Nao wakaendelea kumiliki kazi ngumu ya vikundi vya mataifa,+
45 Ili wapate kushika masharti yake+
Na kushika sheria zake.+
Msifuni Yah!+