10 “Na itatukia kwamba Yehova Mungu wako atakapokuleta katika nchi ambayo aliwaapia mababu zako Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwamba atakupa,+ majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo wewe hukuyajenga,+
23 Basi Yoshua akaichukua nchi yote, kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwahidi Musa,+ kisha Yoshua akawapa Israeli iwe urithi wao kulingana na mafungu yao, kulingana na makabila yao.+ Na nchi haikusumbuliwa na vita tena.+
22 “Nawe ukawapa falme+ na vikundi vya watu, ukawagawia fungu kwa fungu;+ hivi kwamba wakamiliki nchi ya Sihoni,+ nchi ya mfalme wa Heshboni,+ na nchi ya Ogu+ mfalme wa Bashani.+
45 Na mababu zetu waliolirithi waliliingiza pamoja na Yoshua+ ndani ya nchi iliyomilikiwa na mataifa,+ ambayo Mungu aliyafukuza kutoka mbele ya mababu zetu.+ Lilibaki humo mpaka siku za Daudi.