135 Msifuni Yah!+
Lisifuni jina la Yehova,+
Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+
2 Ninyi mnaosimama katika nyumba ya Yehova,+
Katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.+
3 Msifuni Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+
Lipigieni jina lake muziki, kwa maana linapendeza.+
4 Kwa maana Yah amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe,+
Israeli awe mali yake ya pekee.+
5 Kwa maana mimi mwenyewe najua vema kwamba Yehova ni mkuu,+
Na Bwana wetu ni zaidi ya miungu mingine yote.+
6 Kila kitu ambacho Yehova alipendezwa kufanya, amefanya+
Mbinguni na duniani, baharini na katika vilindi vyote vya maji.+
7 Anafanya mivuke ipande kutoka mwisho wa dunia;+
Amefanya hata malango kwa ajili ya mvua;+
Anauleta upepo kutoka katika maghala yake,+
8 Yeye aliyewapiga na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri,+
Mwanadamu na pia mnyama.+
9 Alituma ishara na miujiza katikati yako, Ee Misri,+
Juu ya Farao na juu ya watumishi wake wote;+
10 Yeye aliyepiga mataifa mengi+
Na kuua wafalme wenye nguvu,+
11 Naam, Sihoni mfame wa Waamori+
Na Ogu mfalme wa Bashani+
Na falme zote za Kanaani,+
12 Na ambaye aliitoa nchi yao iwe urithi,+
Urithi kwa Israeli watu wake.+
13 Ee Yehova, jina lako ni la mpaka wakati usio na kipimo.+
Ee Yehova, ukumbusho wako ni wa mpaka kizazi baada ya kizazi.+
14 Kwa maana Yehova atawatetea watu wake,+
Naye atajuta kwa sababu ya watumishi wake.+
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu,+
Kazi ya mikono ya mtu wa udongo.+
16 Zina kinywa, lakini haziwezi kusema lolote;+
Zina macho, lakini haziwezi kuona chochote;+
17 Zina masikio, lakini haziwezi kusikia lolote.+
Pia hazina roho yoyote katika vinywa vyao.+
18 Wale wanaozifanya watakuwa tu kama hizo,+
Kila mtu anayezitegemea.+
19 Ee nyumba ya Israeli, mbarikini Yehova.+
Ee nyumba ya Haruni, mbarikini Yehova.+
20 Ee nyumba ya Lawi, mbarikini Yehova.+
Ninyi mnaomwogopa Yehova, mbarikini Yehova+.
21 Na abarikiwe Yehova kutoka Sayuni,+
Anayekaa katika Yerusalemu.+
Msifuni Yah!+