Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 7:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Musa na Haruni wakafanya hivyo mara moja,+ kama vile Yehova alivyokuwa ameamuru,+ naye akainua fimbo na kuyapiga maji ya Mto Nile machoni pa Farao na watumishi wake,+ nayo maji yote yaliyokuwa katika Mto Nile yakageuzwa kuwa damu.+

  • Kutoka 8:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ndipo Haruni akaunyoosha mkono wake juu ya maji ya Misri, na vyura wakaanza kuja juu na kuifunika nchi ya Misri.

  • Kutoka 8:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Nao wakafanya hivyo. Kwa hiyo Haruni akaunyoosha mkono wake pamoja na fimbo yake na kuyapiga mavumbi ya dunia, nao chawa wakawa juu ya wanadamu na wanyama. Mavumbi yote ya dunia yakawa chawa katika nchi yote ya Misri.+

  • Kutoka 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Basi Yehova akafanya jambo hilo siku iliyofuata, na aina zote za mifugo ya Wamisri zikaanza kufa;+ lakini hakuna mnyama yeyote kati ya mifugo ya wana wa Israeli aliyekufa.

  • Kutoka 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Basi wakachukua masizi ya tanuru na kusimama mbele ya Farao, naye Musa akayarusha kuelekea mbinguni, nayo yakawa majipu yenye malengelenge,+ yanayopasuka juu ya mwanadamu na mnyama.

  • Kutoka 9:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Kwa hiyo Musa akainyoosha fimbo yake kuelekea mbinguni; na Yehova akatoa mingurumo na mvua ya mawe,+ na moto ulikuwa ukishuka chini mpaka duniani, naye Yehova akafanya mvua ya mawe iendelee kunyesha juu ya nchi ya Misri.

  • Kutoka 10:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Sasa Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe+ mkono wako juu ya nchi ya Misri kwa ajili ya nzige, ili waje juu ya nchi ya Misri na kula mimea yote ya nchi, kila kitu ambacho ile mvua ya mawe iliacha.”+

  • Kutoka 10:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe mkono wako kuelekea mbinguni,+ ili giza lipate kutokea juu ya nchi ya Misri nalo giza liweze kuguswa.”

  • Kumbukumbu la Torati 4:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Au je, Mungu alijaribu kuja kuchukua taifa kwa ajili yake mwenyewe kutoka kati ya taifa lingine kwa uthibitisho,+ kwa ishara+ na kwa miujiza+ na kwa vita+ na kwa mkono wenye nguvu+ na kwa mkono ulionyooshwa+ na kwa woga mkuu+ kama yote ambayo Yehova Mungu wenu amewafanyia ninyi katika Misri mbele ya macho yako?

  • Nehemia 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Ndipo ukatoa ishara na miujiza juu ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa nchi yake,+ kwa maana ulijua kwamba walitenda kwa kimbelembele+ juu yao; nawe ukajifanyia jina+ kama ilivyo leo hii.

  • Zaburi 105:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Wakaweka kati yao mambo ya ishara zake,+

      Na miujiza katika nchi ya Hamu.+

  • Matendo 7:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Mtu huyo aliwaongoza watoke+ baada ya kufanya mambo ya ajabu na ishara katika Misri+ na katika Bahari Nyekundu+ na katika nyika kwa miaka 40.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki