Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 27:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 “‘Na kila sehemu ya kumi+ ya nchi, kutoka katika mbegu ya nchi na tunda la mti, ni ya Yehova. Ni kitu kitakatifu kwa Yehova.

  • 2 Mambo ya Nyakati 31:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Na mara tu lile neno lilipoenea, wana wa Israeli+ wakazidisha mazao ya kwanza ya nafaka,+ divai mpya,+ na mafuta+ na asali+ na mazao yote ya shamba,+ nao wakaleta kwa wingi sehemu ya kumi ya kila kitu.+

  • Nehemia 10:37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Pia, mazao ya kwanza ya unga wetu wenye chenga-chenga+ na michango+ yetu na matunda ya kila namna ya mti,+ divai mpya+ na mafuta+ inatupasa tulete kwa makuhani katika majumba ya kulia chakula+ ya nyumba ya Mungu wetu, pia sehemu ya kumi kutoka katika udongo wetu tuwaletee Walawi,+ kwa maana wao, Walawi, ndio hupokea sehemu ya kumi katika majiji yetu yote ya kilimo.

  • Nehemia 12:44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 Tena wanaume wakawekwa siku hiyo juu ya majumba+ ya maghala,+ ya michango,+ ya mazao ya kwanza+ na ya sehemu za kumi,+ ili kukusanya ndani yake mafungu yaliyohitajiwa na sheria+ kutoka katika mashamba ya majiji kwa ajili ya makuhani na Walawi;+ kwa maana shangwe ya Yuda ilitokana na makuhani na Walawi+ waliokuwa wakihudumu.

  • Nehemia 13:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Na Yuda wote wakaleta ndani ya maghala+ sehemu ya kumi+ ya nafaka+ na ya divai mpya+ na ya mafuta.+

  • Wagalatia 6:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Zaidi ya hayo, mtu yeyote anayefundishwa neno kwa mdomo+ na ashiriki+ katika mambo yote mema pamoja na yule anayetoa fundisho hilo la mdomo.+

  • Waebrania 7:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Ni kweli, watu kutoka katika wana wa Lawi+ ambao hupokea cheo chao cha ukuhani wana amri ya kukusanya sehemu za kumi+ kutoka kwa watu+ kulingana na Sheria, yaani, kutoka kwa ndugu zao, hata kama hao wametoka katika viuno vya Abrahamu;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki