7 Nao wana wa Yakobo wakaingia kutoka shambani mara tu waliposikia juu ya hilo; na hao wanaume wakaumia hisia zao, wakakasirika sana,+ kwa sababu alikuwa amefanya upumbavu wenye kufedhehesha juu ya Israeli kwa kulala na binti ya Yakobo,+ wakati ambapo jambo kama hilo halipasi kufanywa.+
23 Ndipo mwenye nyumba akatoka nje, akawaendea na kuwaambia:+ “Hapana, ndugu zangu,+ tafadhali msifanye jambo lolote baya, kwa kuwa mtu huyu ameingia nyumbani mwangu. Msitende upumbavu huu wenye kufedhehesha.+
25 Lakini wanaume hao hawakutaka kumsikiliza. Basi mtu huyo akamchukua suria+ wake na kumleta kwao nje; nao wakaanza kulala na mwanamke huyo,+ wakaendelea kumtendea vibaya+ usiku wote mpaka asubuhi, kisha wakamwacha aende wakati wa mapambazuko.
12 Hata hivyo, yeye akamwambia: “Hapana, ndugu yangu! Usinifedheheshe;+ kwa maana si kawaida kufanya hivi katika Israeli.+ Usifanye upumbavu huu wenye kufedhehesha.+