19 Naye Samweli akamjibu Sauli na kusema: “Mimi ndiye mwonaji. Panda mbele yangu, uende mahali pa juu, nanyi mtakula pamoja nami leo,+ nami nitawaacha mwende zenu asubuhi, nami nitakuambia mambo yote yaliyo moyoni mwako.+
27 Na mfalme akaendelea kumwambia Sadoki kuhani: “Wewe ni mwonaji, sivyo?+ Rudi jijini kwa amani, na pia Ahimaazi mwana wako na Yonathani+ mwana wa Abiathari, wana wenu wawili, pamoja nanyi.
22 Wote waliochaguliwa kuwa watunza-malango kwenye milango walikuwa mia mbili kumi na wawili. Walikuwa katika makao+ yao kulingana na maandikisho yao ya kiukoo.+ Daudi+ na Samweli mwonaji+ waliwaagiza hao rasmi katika vyeo vyao vya kutegemewa.+
29 Na mambo ya Daudi mfalme, ya kwanza na ya mwisho, yameandikwa katika maneno ya Samweli mwonaji+ na katika maneno ya nabii Nathani+ na katika maneno ya Gadi+ mwonaji,