16 “Karibu wakati kama huu kesho nitatuma mtu kwako kutoka katika nchi ya Benyamini,+ nawe umtie mafuta+ awe kiongozi juu ya watu wangu Israeli; naye atawaokoa watu wangu kutoka mkononi mwa Wafilisti,+ kwa sababu nimeona mateso ya watu wangu, kwa maana kilio chao kimenifikia.”+
10Ndipo Samweli akachukua chupa+ ya mafuta na kuyamimina juu ya kichwa chake, akambusu+ na kusema: “Je, si kwa sababu Yehova amekutia mafuta uwe kiongozi+ juu ya urithi wake?+
6 Basi akawaambia watu wake: “Ni jambo lisilowaziwa kwangu, kwa maoni ya Yehova, kwamba nimfanyie bwana wangu jambo hili, mtiwa-mafuta+ wa Yehova, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mtiwa-mafuta wa Yehova.”+
27 Ijapokuwa hivyo, Herode na pia Pontio Pilato+ pamoja na watu wa mataifa na pamoja na vikundi vya watu wa Israeli kwa kweli walikusanyika pamoja katika jiji hili dhidi ya mtumishi wako mtakatifu+ Yesu, ambaye ulimtia mafuta,+
38 yaani, Yesu aliyekuwa ametoka Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa roho takatifu+ na nguvu, naye akaenda akipita katika nchi akitenda mema na kuwaponya wote waliokandamizwa na Ibilisi;+ kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.+