51 Na Daudi akaendelea kukimbia, akasimama juu ya yule Mfilisti. Halafu akachukua upanga wake+ na kuuchomoa kutoka ndani ya ala yake, na kumuua kabisa alipoutumia kukikata kichwa chake.+ Nao Wafilisti wakaona kwamba mwanamume wao mwenye nguvu amekufa, nao wakaanza kukimbia.+
9 Nao wakakata kichwa+ chake na kuvua silaha zake na kutuma wajumbe kotekote katika nchi ya Wafilisti ili kuzijulisha+ nyumba za sanamu+ zao pamoja na watu.
7 Na ikawa kwamba mara tu barua ile ilipowafikia, wakawachukua wale wana wa mfalme na kuwachinja, watu 70,+ kisha wakaviweka vichwa vyao ndani ya vikapu, wakampelekea kule Yezreeli.