23 Lakini akaendelea kukataa kugeuka kando; ndipo Abneri akampiga tumboni+ kwa ncha ya nyuma ya mkuki, hata mkuki ukatokea upande wake wa nyuma; akaanguka hapo, akafa papo hapo. Na ikawa kwamba watu wote waliofika mahali ambapo Asaheli alianguka kisha akafa wakawa wakisimama tuli.+