15 “Naye Haruni na wanawe watamaliza kufunika mahali patakatifu+ na vyombo+ vyote vya mahali patakatifu wakati kambi inapoondoka, kisha wana wa Kohathi watakuja ili kuvichukua,+ lakini hawapaswi kugusa+ mahali patakatifu wasije wakafa. Vitu hivyo ni mzigo wa wana wa Kohathi katika hema la mkutano.+
3 wakawaamuru watu, wakisema: “Mara mtakapoliona sanduku la agano la Yehova Mungu wenu, na makuhani Walawi wakiwa wamelichukua,+ ndipo mtakapoondoka mahali penu, nanyi mlifuate,
2 Ndipo Daudi aliposema: “Mtu yeyote asilibebe sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua hao ili walibebe sanduku la Yehova+ na kumhudumia+ mpaka wakati usio na kipimo.”
15 Ndipo wana wa Walawi wakaanza kulibeba+ sanduku la Mungu wa kweli, kama Musa alivyoamuru kwa amri ya Yehova, juu ya mabega yao na fimbo zikiwa juu yao.+