20 “Hata hivyo, nabii atakayethubutu kusema katika jina langu neno ambalo sijamwamuru kusema+ au atakayesema katika jina la miungu mingine,+ nabii huyo lazima afe.+
16 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatolea ninyi unabii.+ Wanawafanya muwe ubatili.+ Wanasema maono ya moyo wao wenyewe+—si kutoka katika kinywa cha Yehova.+
17 Wanawaambia tena na tena wale ambao hawaniheshimu, ‘Yehova amesema: “Ninyi mtakuwa na amani.”’+ Nao wamemwambia kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake,+ ‘Hamtapatwa na msiba wowote.’+
6 “Wameona maono ya jambo lisilo la kweli na uaguzi wa uwongo,+ wale wanaosema, ‘Neno la Yehova ni,’ wakati ambapo Yehova mwenyewe hajawatuma, nao wamengoja neno litimie.+