Kumbukumbu la Torati
18 “Hakuna fungu au urithi pamoja na Israeli litakalokuja kuwa la makuhani, Walawi,+ kabila zima la Lawi. Matoleo yanayotolewa kwa njia ya moto kwa Yehova, naam, urithi wake, watayala.+ 2 Kwa hiyo hakuna urithi utakaokuja kuwa wake katikati ya ndugu zake. Yehova ndiye urithi wake,+ kama vile alivyosema naye.
3 “Sasa hii itaendelea kuwa haki wanayostahili makuhani kutoka kwa watu, kutoka kwa wale wanaotoa dhabihu, iwe ni ng’ombe-dume au kondoo: Mtu atampa kuhani mfupa wa bega na mataya na tumbo. 4 Sehemu ya kwanza ya nafaka yako, divai yako mpya na mafuta yako na sufu yako ya kwanza iliyokatwa ya kundi lako unapaswa kumpa.+ 5 Kwa maana yeye ndiye ambaye Yehova Mungu wako amechagua kutoka kati ya makabila yako yote, asimame ili kuhudumu katika jina la Yehova, yeye na wanawe, sikuzote.+
6 “Na ikiwa Mlawi ataenda nje ya moja la majiji yako ya Israeli yote, ambapo alikaa kwa muda,+ naye aje kwa sababu ya tamaa yoyote ya nafsi yake mpaka mahali ambapo Yehova atapachagua,+ 7 atahudumu pia katika jina la Yehova Mungu wake sawa na ndugu zake wote, Walawi, wanaosimama hapo mbele za Yehova.+ 8 Atakula fungu linalolingana,+ mbali na kile anachopata kutokana na vitu anavyouza kati ya mali za mababu zake.
9 “Utakapokuwa umeingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe, usijifunze kufanya kulingana na machukizo ya mataifa hayo.+ 10 Asipatikane ndani yako yeyote anayempitisha mwana wake au binti yake katikati ya moto,+ yeyote anayefanya uaguzi,+ mwenye kufanya uchawi+ au yeyote anayetafuta ishara za bahati+ au mlozi,+ 11 au anayefunga wengine kwa kuwatakia maovu+ au yeyote anayetafuta shauri kwa mwenye kuwasiliana na pepo+ au mjuzi wa kubashiri matukio+ au yeyote anayeuliza habari kutoka kwa wafu.+ 12 Kwa maana kila mtu anayefanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya machukizo hayo, Yehova Mungu wako anawafukuza kutoka mbele yako.+ 13 Utajionyesha kuwa huna kosa kwa Yehova Mungu wako.+
14 “Kwa maana mataifa haya unayoyafukuza yalikuwa yakiwasikiliza wale wanaofanya uchawi+ na wale wanaoagua;+ lakini wewe, Yehova Mungu wako hajakupa kitu chochote kama hicho.+ 15 Nabii kutoka katikati yako mwenyewe, kutoka kwa ndugu zako, kama mimi, ndiye ambaye Yehova Mungu wako atakuinulia—ninyi mnapaswa kumsikiliza yeye+— 16 kulingana na yote uliyomwomba Yehova Mungu wako huko Horebu katika ile siku ya kutaniko,+ na kusema ‘Usiache nisikie tena sauti ya Yehova Mungu wangu, na huu moto mkubwa usiache niuone tena, nisije nikafa.’+ 17 Ndipo Yehova akaniambia, ‘Wamefanya vema katika kusema walilosema.+ 18 Nitawainulia wao nabii kutoka katikati ya ndugu zao, kama wewe;+ nami nitaweka maneno yangu katika kinywa chake,+ naye atasema nao yote nitakayomwamuru.+ 19 Na itatukia kwamba mtu ambaye hatasikiliza maneno yangu ambayo atayasema katika jina langu, mimi mwenyewe nitamtaka ajibu.+
20 “Hata hivyo, nabii atakayethubutu kusema katika jina langu neno ambalo sijamwamuru kusema+ au atakayesema katika jina la miungu mingine,+ nabii huyo lazima afe.+ 21 Na ikiwa utasema moyoni mwako: “Tutajuaje neno ambalo Yehova hajasema?”+ 22 Nabii anaposema katika jina la Yehova na neno hilo lisitukie au lisitimie, hilo ndilo neno ambalo Yehova hakusema.+ Kwa kimbelembele nabii huyo alilisema. Usimwogope.’+