14 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Manabii wanatoa unabii wa uwongo katika jina langu.+ Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru wala kusema nao.+ Maono ya uwongo na uaguzi na kitu kisicho na thamani+ na udanganyifu wa moyo wao ndiyo mambo wanayowaambia ninyi kwa njia ya unabii.+
15 Na Yeremia nabii akaendelea kumwambia Hanania+ nabii: “Tafadhali, sikiliza, Ee Hanania! Yehova hakukutuma wewe, bali wewe mwenyewe umewafanya watu hawa wautegemee uwongo.+
3 Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Ole wao manabii wajinga,+ wanaoifuata roho yao wenyewe,+ wakati ambapo hakuna chochote ambacho wameona!+
28 Nao manabii wake wamewapigia lipu kwa kutumia chokaa,+ wakiona maono yasiyo halisi+ na kuagua uwongo+ kwa ajili yao, na kusema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi,” wakati ambapo Yehova mwenyewe hajasema.