14 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Manabii wanatoa unabii wa uwongo katika jina langu.+ Mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru wala kusema nao.+ Maono ya uwongo na uaguzi na kitu kisicho na thamani+ na udanganyifu wa moyo wao ndiyo mambo wanayowaambia ninyi kwa njia ya unabii.+
15 “‘Kwa maana mimi sikuwatuma,’ asema Yehova, ‘lakini wanatoa unabii katika jina langu kwa uwongo, kusudi niwatawanye,+ nanyi mwangamie,+ ninyi pamoja na wale manabii wanaowatolea unabii.’”+
31 “Tuma ujumbe kwa watu wote waliohamishwa,+ ukisema, ‘Yehova amesema hivi kumhusu Shemaya wa Nehelamu: “Kwa sababu Shemaya amewatolea ninyi unabii, lakini mimi mwenyewe sikumtuma, naye alijaribu kuwafanya mtegemee uwongo,+
3 Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Ole wao manabii wajinga,+ wanaoifuata roho yao wenyewe,+ wakati ambapo hakuna chochote ambacho wameona!+
3 Na itatukia kwamba mtu akitoa unabii tena, baba yake na mama yake, waliomzaa, watamwambia pia, ‘Wewe hutaishi, kwa maana umesema uwongo katika jina la Yehova.’ Na baba yake na mama yake, waliomzaa, watamchoma kwa silaha kwa sababu ametoa unabii.+