22 Nabii anaposema katika jina la Yehova na neno hilo lisitukie au lisitimie, hilo ndilo neno ambalo Yehova hakusema.+ Kwa kimbelembele nabii huyo alilisema. Usimwogope.’+
13 “Kwa maana kuanzia aliye mdogo zaidi kati yao mpaka aliye mkubwa zaidi kati yao, kila mmoja anajipatia pato lisilo la haki;+ na kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa uwongo.+
2 “Mwana wa binadamu, toa unabii kuwahusu manabii wa Israeli wanaotoa unabii,+ nawe utawaambia wale wanaotoa unabii kutoka moyoni mwao wenyewe,+ ‘Sikieni neno la Yehova.+
4 “Na itatukia katika siku hiyo kwamba manabii wataona aibu,+ kila mmoja kwa sababu ya maono yake anapotoa unabii; nao hawatavaa vazi rasmi la manyoya+ kwa kusudi la kudanganya.