Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 2:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Makuhani wenyewe hawakusema, ‘Yehova yuko wapi?’+ Na wale wanaoshughulika na sheria hawakunijua;+ na wachungaji wenyewe walinikosea,+ na hata manabii walitoa unabii kupitia Baali,+ nao wakawafuata wale ambao hawangeweza kuleta faida yoyote.+

  • Yeremia 14:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kwa kweli nikienda nje shambani, tazama, sasa, wale waliouawa kwa upanga!+ Na kwa kweli mimi nikija ndani ya jiji, tazama, pia, magonjwa yaliyoletwa na njaa!+ Kwa maana nabii na kuhani vilevile wamezunguka kwenda katika nchi ambayo hawakuijua.’”+

  • Yeremia 23:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “Kwa maana nabii pamoja na kuhani wametiwa unajisi.+ Pia katika nyumba yangu mwenyewe nimeupata ubaya wao,”+ asema Yehova.

  • Mika 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Yehova amesema hivi juu ya manabii ambao wanawapoteza watu wangu,+ ambao wanauma kwa meno yao+ na ambao hupaaza sauti, ‘Amani!’+ ambao, mtu yeyote asipoweka kitu vinywani mwao, pia hutakasa vita juu yake,+

  • Mika 3:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Walio vichwa vyake hutoa hukumu ili wale rushwa+ tu, na makuhani wake hufundisha ili tu wapate malipo,+ na manabii wake hufanya uaguzi ili tu wapate pesa;+ hata hivyo wao huendelea kujiegemeza kwa Yehova, wakisema: “Je, Yehova hayuko katikati yetu?+ Hakuna msiba utakaotupata.”+

  • Sefania 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Manabii wake walikuwa na dharau, walikuwa watu wenye hila.+ Makuhani wake wamekitia unajisi kilicho kitakatifu; waliitendea sheria jeuri.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki