14 Hata wakuu wote wa makuhani+ na watu wenyewe wakatenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa kiasi kikubwa, kulingana na machukizo+ yote ya mataifa, hivi kwamba wakaitia unajisi nyumba ya Yehova aliyokuwa ameitakasa katika Yerusalemu.+
11 Je, nyumba hii ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ imekuwa pango tu la wanyang’anyi machoni penu?+ Tazama, mimi mwenyewe pia nimeona jambo hilo,” asema Yehova.+
11 Na wanaume 70+ wazee wa nyumba ya Israeli, pamoja na Yaazania mwana wa Shafani+ akiwa amesimama kati yao, walikuwa wamesimama mbele ya hiyo, kila mmoja akiwa na chetezo chake mkononi mwake, na manukato ya wingu la uvumba yalikuwa yakipaa.+
39 Nao walipokuwa wamewachinja wana wao kwa ajili ya sanamu zao za mavi+ waliingia ndani ya patakatifu pangu katika siku hiyo ili kupatia unajisi,+ na, tazama! hivyo ndivyo wamefanya katikati ya nyumba yangu.+