10 Nao hawakuwafukuza Wakanaani+ waliokuwa wakikaa katika Gezeri,+ na Wakanaani hao huendelea kukaa katikati ya Efraimu mpaka leo hii,+ nao wakawa watumishi wa kazi ya kulazimishwa.+
13 Na ikawa kwamba wakati wana wa Israeli walipokuwa wamepata nguvu,+ wakawaweka Wakanaani wafanye kazi ya kulazimishwa,+ wala hawakuwafukuza kikamilifu.+
22 Na Sulemani hakumfanya yeyote kati ya wana wa Israeli kuwa mtumwa;+ kwa maana wao walikuwa ndio mashujaa wa vita na watumishi wake na wakuu wake na maamiri wasaidizi wake na wakuu wa waendesha-magari wake na wakuu wa wapanda-farasi wake.+
9 Lakini Sulemani hakumfanya yeyote kati ya wana wa Israeli kuwa mtumwa kwa ajili ya kazi yake;+ kwa maana hao walikuwa mashujaa wa vita+ na wakuu wa maamiri wake wasaidizi na wakuu wa waendesha-magari+ wake na wakuu wa wapanda-farasi+ wake.