Yoshua
16 Na kura+ ya wana wa Yosefu+ ikawa kutoka Yordani+ huko Yeriko hadi kwenye maji ya Yeriko upande wa mashariki, nyika inayopanda kutoka Yeriko hadi katika eneo lenye milima la Betheli.+ 2 Na ikatoka Betheli, iliyokuwa ya Luzi+ na kwenda hadi kwenye mpaka wa Waarki+ huko Atarothi, 3 nayo ikashuka kwenda magharibi hadi kwenye mpaka wa Wayafleti hadi kwenye mpaka wa Beth-horoni+ ya Chini na Gezeri,+ na mwisho wake ukawa kwenye bahari.+
4 Na wana wa Yosefu,+ Manase na Efraimu,+ wakaanza kuimiliki nchi.+ 5 Na mpaka wa wana wa Efraimu kulingana na familia zao ulikuwa, ndiyo, mpaka wa urithi wao upande wa mashariki ulikuwa Ataroth-adari,+ hadi Beth-horoni ya Juu;+ 6 na mpaka huo ukaenda hadi baharini. Mikmethathi+ ilikuwa upande wa kaskazini, na mpaka huo ukazunguka upande wa mashariki hadi Taanath-shilo, ukaenda upande wa mashariki hadi Yanoa. 7 Nao ukashuka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara ukafika Yeriko+ na kwenda hadi Yordani. 8 Kutoka Tapua+ mpaka huo ukaendelea upande wa magharibi hadi kwenye bonde la mto la Kana,+ na mwisho wake ukawa kwenye bahari.+ Huo ndio urithi wa kabila la wana wa Efraimu kulingana na familia zao. 9 Na wana wa Efraimu walikuwa na majiji yaliyozungukwa+ katikati ya urithi wa wana wa Manase, majiji yote na makao yake.
10 Nao hawakuwafukuza Wakanaani+ waliokuwa wakikaa katika Gezeri,+ na Wakanaani hao huendelea kukaa katikati ya Efraimu mpaka leo hii,+ nao wakawa watumishi wa kazi ya kulazimishwa.+