19 Zaidi ya hayo, akawagawia+ watu wote, umati wote wa Israeli, mwanamume na mwanamke vilevile, kila mmoja keki ya mkate ya mviringo na keki ya tende na keki ya zabibu kavu,+ kisha watu wote wakaenda, kila mmoja nyumbani kwake.
66 Katika siku ya nane akawaacha watu waende zao;+ nao wakaanza kumbariki mfalme na kwenda kwenye nyumba zao, wakishangilia+ na kufurahi moyoni+ mwao kutokana na wema+ wote ambao Yehova alikuwa ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na kwa ajili ya Israeli watu wake.