9 Nao wakaanza kufundisha+ katika Yuda, nao walikuwa na kitabu cha sheria ya Yehova;+ nao wakaendelea kuzunguka katika majiji yote ya Yuda na kufundisha kati ya watu.
3 Naye akaendelea kusoma+ ndani ya kile kitabu kwa sauti mbele ya kiwanja cha watu wote kilichoko mbele ya Lango la Maji, kuanzia mapambazuko+ mpaka katikati ya mchana, mbele ya wanaume na wanawake na mbele ya wale wengine wenye akili; na watu wote wakasikiliza+ kwa makini+ kitabu cha sheria.
7 Kwa maana midomo ya kuhani ndiyo inayopaswa kutunza ujuzi, na sheria ndiyo ambayo watu wanapaswa kutafuta kutoka kinywani mwake;+ kwa maana yeye ndiye mjumbe wa Yehova wa majeshi.+
52 Ndipo akawaambia: “Ikiwa ni hivyo, kila mfundishaji wa watu wote, anapofundishwa kuhusiana na ufalme wa mbinguni,+ ni kama mtu, mwenye nyumba, ambaye hutoa katika hazina yake vitu vipya na vya zamani.”+