-
Esta 3:12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Ndipo waandishi+ wa mfalme wakaitwa katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na tatu ya mwezi huo. Basi kuandika+ kukaendelea kulingana na yote ambayo Hamani aliwaamuru maliwali wa mfalme na magavana waliokuwa juu ya wilaya mbalimbali za utawala,+ na wakuu wa vikundi mbalimbali vya watu, wa kila wilaya ya utawala, katika mtindo wao wa kuandika,+ na kila kikundi cha watu kwa lugha yao wenyewe. Hayo yaliandikwa kwa jina+ la Mfalme Ahasuero na kutiwa muhuri kwa pete+ ya mfalme.
-
-
Esta 8:5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Sasa akasema: “Ikiwa inaonekana vema kwa mfalme, na ikiwa nimepata kibali+ mbele yake na jambo hili linafaa mbele ya mfalme nami ni mwema machoni pake, na iandikwe kwamba zile barua zifutwe,+ ule mpango wa hila wa Hamani mwana wa Hamedatha Mwagagi,+ ambazo aliandika kuwaangamiza Wayahudi+ walio katika wilaya zote za utawala+ wa mfalme.
-