31 “Nami nitauweka mpaka wako kutoka Bahari Nyekundu hadi bahari ya Wafilisti na kutoka nyikani hadi kwenye Mto;+ kwa sababu nitawaweka wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, na hakika wewe utawafukuzia mbali kutoka mbele yako.+
21 Naye Sulemani alikuwa mtawala juu ya falme zote kutoka ule Mto+ hadi kwenye nchi ya Wafilisti na hadi kwenye mpaka wa Misri. Walikuwa wakileta zawadi na kumtumikia Sulemani siku zote za maisha yake.+
10 Nami nitalikatilia mbali gari la vita kutoka katika Efraimu na farasi kutoka katika Yerusalemu.+ Na upinde wa mapigano+ utakatiliwa mbali. Naye atasema amani kwa mataifa;+ na utawala wake utakuwa kutoka bahari mpaka bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.+