8 Tazama, ninawaleta kutoka katika nchi ya kaskazini,+ nami nitawakusanya kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+ Kati yao patakuwa na vipofu na vilema, mwanamke mwenye mimba na yule anayezaa, wote pamoja.+ Watarudi hapa wakiwa kutaniko kubwa.+
27 Nitakapowarudisha kutoka katika vikundi vya watu nami kwa kweli niwakusanye pamoja kutoka katika nchi za adui zao,+ mimi pia nitajitakasa mwenyewe katikati yao mbele ya macho ya mataifa mengi.’+
29 Zaidi ya hayo, watu watakuja kutoka sehemu za mashariki na za magharibi, na kutoka kaskazini na kusini,+ nao wataketi mezani katika ufalme wa Mungu.+