Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 13:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Lakini mke wake akamwambia: “Ikiwa Yehova alitaka tu kutuua, basi hangekubali toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka kutoka mkononi mwetu,+ naye hangetuonyesha mambo haya yote, naye kufikia sasa hangetuacha tusikie jambo lolote kama hili.”+

  • 1 Samweli 25:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Na usiache hili liwe kwako sababu ya kufadhaika wala kikwazo kwa moyo wa bwana wangu, kwa kumwaga damu bila sababu+ na pia kwa kuacha mkono wa bwana wangu mwenyewe umwokoe.+ Na hakika Yehova atamfanyia mema bwana wangu, nawe utamkumbuka+ kijakazi wako.”

  • 2 Samweli 20:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Na mwanamke fulani mwenye hekima+ akaanza kuita kutoka jijini: “Sikilizeni, sikilizeni! Tafadhali, mwambieni Yoabu, ‘Njoo karibu mpaka hapa, nami niseme na wewe.’”

  • Esta 5:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Ikiwa nimepata kibali machoni pa mfalme,+ na ikiwa inaonekana vema kwa mfalme kunipa haja yangu na kufanya kulingana na ombi langu, mfalme pamoja na Hamani na waje kwenye karamu ambayo nitawafanyia kesho, nami kesho nitafanya kulingana na neno la mfalme.”+

  • Zaburi 68:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova mwenyewe anasema neno hili;+

      Wanawake wanaotangaza habari njema ni jeshi kubwa.+

  • Methali 31:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Maneno ya Lemueli mfalme, ujumbe mzito+ ambao mama yake alimwambia ili kumrekebisha:+

  • Matendo 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Na mwanamume huyo akaanza kusema kwa ujasiri katika sinagogi. Prisila na Akila+ walipomsikia, wakamchukua na kumfafanulia kwa usahihi zaidi njia ya Mungu.

  • Tito 2:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Vivyo hivyo wanawake wenye umri mkubwa+ wawe wenye tabia ya kumhofu Mungu, si wachongezi,+ wala si watumwa wa divai nyingi sana, wawe walimu wa yaliyo mema;

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki