6 Wakati huo kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya,+ na ulimi wa bubu utapaaza sauti kwa furaha.+ Kwa maana maji yatakuwa yamebubujika katika nyika, na mito katika nchi tambarare ya jangwani.
18 Nitafungua mito juu ya vilima vitupu, na mabubujiko katikati ya nchi tambarare za bondeni.+ Nitaifanya nyika kuwa dimbwi la maji lenye matete mengi, na nchi isiyo na maji kuwa chemchemi za maji.+
11 Na Yehova hatakosa kukuongoza+ sikuzote+ na kuishibisha nafsi yako hata katika nchi yenye kukauka,+ naye ataitia nguvu mifupa yako;+ nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+ na kama chemchemi ya maji, ambayo maji yake hayaishi.