8 Na hakika kutakuwa na njia kuu hapo,+ ndiyo, njia; nayo itaitwa Njia ya Utakatifu.+ Asiye safi hatapita juu yake.+ Nayo itakuwa kwa ajili ya yule anayetembea katika njia hiyo, wala hakuna wapumbavu watakaotembea huku na huku juu yake.
21 Na kwa habari ya watu wako, wote watakuwa waadilifu;+ mpaka wakati usio na kipimo wataimiliki nchi,+ chipukizi nililolipanda,+ kazi ya mikono yangu,+ ili mimi nirembeshwe.+
15 “Tazama! Milimani, miguu ya mtu anayeleta habari njema, anayetangaza amani.+ Ee Yuda, fanya sherehe zako.+ Timiza nadhiri zako;+ kwa sababu mtu yeyote asiyefaa kitu hatapita tena kamwe katikati yako.+ Hatakosa kukatiliwa mbali kabisa.”+
27 Lakini kitu chochote kisicho kitakatifu na yeyote anayeendelea kutenda chukizo+ na uwongo+ hataingia ndani yake hata kidogo;+ watakaoingia ni wale tu walioandikwa katika kile kitabu cha kukunjwa cha uzima cha Mwana-Kondoo.+