-
Kumbukumbu la Torati 31:17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Ndipo hasira yangu itakapowaka kwelikweli juu yao katika siku hiyo,+ nami hakika nitawaacha+ na kuuficha uso wangu mbali nao,+ nao watakuwa kitu cha kuteketezwa; na misiba mingi na taabu zitakuja juu yao,+ nao watalazimika kusema siku hiyo, ‘Je, misiba hii haikuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko katikati yetu?’+
-
-
Ezekieli 39:23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba ilikuwa kwa sababu ya kosa lao kwamba wao, nyumba ya Israeli, walienda uhamishoni,+ kwa sababu walijiendesha kwa kukosa uaminifu kunielekea mimi, hivi kwamba nikawaficha wao uso wangu+ na kuwatia mkononi mwa wapinzani wao, nao wakawa wakianguka, wote hao, kwa upanga.+
-