Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 31:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Ndipo hasira yangu itakapowaka kwelikweli juu yao katika siku hiyo,+ nami hakika nitawaacha+ na kuuficha uso wangu mbali nao,+ nao watakuwa kitu cha kuteketezwa; na misiba mingi na taabu zitakuja juu yao,+ nao watalazimika kusema siku hiyo, ‘Je, misiba hii haikuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko katikati yetu?’+

  • Kumbukumbu la Torati 32:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Kwa hiyo akasema, ‘Acha niufiche uso wangu kutoka kwao,+

      Acha nione mwisho wao utakuwaje baadaye.

      Kwa maana wao ni kizazi chenye upotovu,+

      Wana ambao ndani yao hamna uaminifu.+

  • Ezekieli 39:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba ilikuwa kwa sababu ya kosa lao kwamba wao, nyumba ya Israeli, walienda uhamishoni,+ kwa sababu walijiendesha kwa kukosa uaminifu kunielekea mimi, hivi kwamba nikawaficha wao uso wangu+ na kuwatia mkononi mwa wapinzani wao, nao wakawa wakianguka, wote hao, kwa upanga.+

  • Mika 3:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Wakati huo watamwomba Yehova msaada, lakini hatawajibu.+ Naye atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo,+ kulingana na walivyotenda ubaya kwa matendo yao.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki